Tuesday, September 8, 2009

BSS walivyoleta 'njaa' kwa mashabiki


Mwishoni mwa wiki kulikuwa na kazi temeke, baada ya kwenda Mlimani na Coco Beach kwa washua, watoto wa BSS walijaiachia TCC Chang'ombe na shoo ikawa kama hivi.
Huyo ni Beatrice

Sarafina naye alikuwepo...

Paschal naye kazini...

George aliwakilisha kihivi...

..Mwapwwani na mambo yake yaleeee...

Mtu mzima Msechu naye kazini...

Kisha kwa pamoja wakangia uwanjani...

..na Nyomi lilikuwa kihivi baaab!

Watoto wa Ilala


Mabinti kutoka Ilala wakijinadi kuliwakilisha vilivyo jiji la Dar es salaam katika kambi ya Miss Tanzania ambayo imeanza leo katika Hotel ya Girrafe View Hotel
Kambi ilianza rasmi jana

Yu wapi?


Tangu tusikie amekula shavu la Sony Music amekuwa kimya sana, washakunaku, wakunwaji wa masuala ya muziki na mashabiki wake, kwa pamoja wanaungana na kuuliza, yuko wapi?
Mwenye jibu alete

Sunday, September 6, 2009

BBR Dinner Party, kula haikuwa rahhisi kiviiiile...


Dada Furaha wa Multichoice bwana, leo aliwaambia watu hakuna kula mpaka mmalize kazi, watu ikabidi waingie mzigoni, hii ilikuwa meza yangu, kamanda wetu alikuwa Ambwene Yesaya

Jipangeni wanangu, sio ishu wala nini, kamanda Ambwene akiweka sawa wanawe!

..hatimaye watu wakafanikiwa...

The Revolution 2009


Big Brother nyingine inaanza leo vijana wanaingia kambini kuanzia saa 12 za jioni, tukae tayari...

...na humu, ..ndimo watakamojidai...

He, ..kawa mtangazaji?


Jamani, huyu si yule Charls wa Maisha Plus jama? ..haya nasikia kala shavu Clods TV, ..kaaazi kweli kweli..
Na tuisubiri

Umasaini...


...baada ya kuwapima pima sana warembo, majaji waliokuwa wakipiga misele ya kumtafuta kisura wa Tanzania mwaka huu, misele ambayo imedhaminiwa na Vita Matl Plus wakaamua kuweka pozi, kushoto ni Emmy Melau, Ally Remtullah a.k.a Superstar, na Nashino...
Kazi inaendelea

Mama Sambona


Misoji Nkwabi mshindi wa shindano la Bongo Star Search mwaka jana amemaliza kurekodi tamthilia inayoitwa Mama sambona nchini Ujerumani, kaa tayari kuiona, hapa ni wakati akiwa katika kuitengeneza

Saturday, September 5, 2009

Kwa hisani yenu...


Jamaa anatia huruma jama na tuzo anahitaji, ili kumfanikisha andika neno BHH AY kwenda 0789 777 333
Utakuwa umemsaidia sana

Anafaa?


Timu ya Kisura ikiendelea na kazi, hapa Emmy Melau na Ally Remtullah wakiwa kazini, kazi ilikuwa sio ndogo kama mnavyofikiria wadau

Friday, September 4, 2009

Msako


Msako wa kumtafuta Kisura wa Tanzania ambao mwaka huu uko chini ya udhamini mkubwa wa serengeti Breweries ndio uko kwa mahewa hivi, hapa mtu mzima Mussa nKisoki, shoto kabisa akiongoza timu za BTA na Sofia records kuifanya kazi nzima

Thursday, September 3, 2009

haya, ..huyu hapa! ..looh!


...dah wanazi wa mji walinipa mtihani, eti kama kweli mie nii la Nyeti, niwaoneshe sura ya Babra wa Clouds TV.
..hatimaye huyu hapa, ..Ooouph, haya sen]meni jingine na mkitaka kumuona kwa zaidi subirini Clouds TV, atakuwa anajiachia kwa sana tu

Kazi imeanza....


Nimerudi tena hewani kubwa la maadui a.k.a bedui, ...kudadadeki nimefufuliwa na zain ambayo imeniweka hewani muda wote, ...masaa 23456788 hewani!
...na ishu ninayoanza nayo ni ya Kisura wa Tanzania ambayo mwaka huu imedhaminiwa na Vita Malt, na huyu dada kwenye kamera anaitwa Brighter, ndio ataiendesha shughuli nzima, kaa tayari kuisikia.
Mwabheja sana!

Thursday, June 11, 2009

Noma kweli, subiria kipindi chake...


Hivi hii mwaka gani unakumbuka? Mtu mzima nilitaka kujikakamua nikahisi mnhhhhhhh....
(M'jokin' was just testing the Mic, heee umetoa mimaaaacho mwenyewe!)

..dah shavu...


Watoto wa THT wamekula shavu kutoka Barrick,. kama M 35hv kwa ajili ya kuendeleza vipaji kikiwa ni kituo cha kwanza kupata msaada wa namna hii kutoka taasisi za nyumbani.
Hapo inathibitisha nini, si ndio kwamba wanaweza sana, au mnasemaje wadau?

Baba na Mwana


Jumapili ijayo ya tarehe 21 June ni siku ya wababa, ..eh bwana kizungu inaitwa Fathrrs Day, sasa ona huyu ni Maunda na huyu ni Mzee Zahir Zorro, katika ile ambayo mimi na washkaji zangu tumeipachika jina la Show Luv

Mzee wa Mashinoshino...


Kipindi hiki ndio wachumi huwa wanaumana sana kuhusiana na nini kiwe nini kisiwe katika Bajeti, hapa nimemnasa Cheyo nje ya ukumbi wa Bunge akijadili kitu na Karamagi..

Wednesday, June 10, 2009

Bata la Ushoto...


Kupanda milima ya Ushoto kazi jamani nilikwenda huku mimi na msh'kaji wangu Sarah ambaye ni Meneja wa bia ya Malta na Aaron.
Sarah ilibidi kutiumia fimbo kupanda, ...mcheki


...tukafika Mimi na Sarah


Tukafika hatimaye, Sarah Aron na mimi...

Tuesday, June 9, 2009

Je wajua?


1. Michoro ya kondom iligundulika katika mapango huko Marekani, michoro hiyo ilichorwa miaka 15,000 iliyopita.Hata hivyo haijulikani kondomu za wakati huo zilikuwa zikitengenezwa kwa 'material' gani.

2. Hapo mwanzo kondomu zilikuwa zikitolewa iwapo tu utakuwa umeandikiwa na daktari, wanaume walikuwa wakiandikiwa na daktari watumie kondomu kwa ajili ya kujikinga na magonjwa ya zinaa na wanawake walikuwa wakiandikiwa watumie kondomu ili wasipate ujauzito.

3. Kondomu ya kwanza ya mpira ilitengenezwa mwaka 1855. Zilitengenezwa maalumu kwaajili ya wanajeshi wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Waingereza.

4. Wakati wa vita kuu ya kwanza ya dunia chama cha afya cha Marekani kilikuwa kikipinga matumizi ya kondomu kwa madai kuwa kama mtu ameamua kufanya mapenzi na mwanamke asiyemfahamu anastahili kupata magonjwa ya zinaa.

5. Wakati hapa kwetu ndo tumeingiza mashine za kuuzia kondomu huko mashariki ya mbali mashine hizi zimetimiza miaka 80 tangu zilipoanza kutumika.

6. Kaa tayari kwa kondomu za kupaka, yes unapaka kama mafuta then zinakauka na kuwa kama kondomu uzijiazo, Salama, Dume, Durex n.k. hivi sasa kondomu hizi zinafanyiwa majaribu ya mwisho mwisho kwa taarifa ni kwamba kondomu hizi ninakuwa kama jelly ambayo ukiipaka inapata joto na kukauka.

Mchongo uko hivi...


Mashosti, ...Enikah Bukuku na Carola Kinasha, wakijadili jinsi ya kulivaa jukwaa kabla ya uzinduzi wa albam mseto ya Wa Hapahapa Jumapili ya Juzi, lilikuwa poa sana tamasha...

ShoWluv


Unaambiwa ile kuangalia huku na huku, Abdul wa Maisha Plus si akaibuka? Tukala shot kimtindo...

Malta Guiness Street Dance Africa ya Tanga...


Tanga ilikuwa balaa tulikutana na vijana wanaojua kuzikata ngoma kwa kweli...


...cheki mwenyewe...


Na piaaaaa, ...matonya si alionesha staili mpya za steji shoo?


.....kwa Tanga hawa wanaitwa Faxers bwana walichukua ile kilo sita ya TBL kwa Tanga na wanatarajiwa kuja town mwezi ujaop kwa mashindano ya kimataifa

Wednesday, June 3, 2009

Wa Hapahapa...


Jumapili ya tarehe 7 mwezi huu pale Coco Beach kutakuwa na bonge moja ya Party la uzinduzi wa albam mseto ya Wa Hapahapa, ambapo wanamuziki lukuki wa nyumbani watashiriki, miongoni mwao ni hawa hapa waliokuwa wakiongea nasi hivi karibuni katika Hopteli ya Southern Sun, kutoka kushoto ni Enikah Bukuku, Paul Ndunguru, Frorah Mbasha na Banana Zorro, ...kiingilio ni bure...

Ngwasumaaaz...


FM Academia, wazee wa ngwasuma ndio bendi pekee ya muziki wa dansi ambayo imekula shoo nyingi sana msimu huu wa ulimbwende, hii ni kutokana na ukweli kwamba mshamini wao hana shobo, si unamjua?
Henekeeeeeene, ..kudadadeki!

Mlishtukia?


Amani alikuwepo this weekend ingawa watu walimuona sana Wahu, alikuwa katika Marketers Night ilikuwa poa sana, hivi mlishtukia?

Yalaaaah!


Richie jamani, ...kafa kiflamu? Hii ni katika muvi yake mpya itakayokuwa inajulikana kwa jina la Solemba, kaa mkao wa kuiona...

Tuesday, June 2, 2009

Unamjua fresh Che Guevara?


1. Pamoja na historia ya kuwa jamaa alikuwa akipigania uhuru wa Cuba, hakuwahi kuwa raia wa nchi hiyo, alizaliwa Argentina lakini pia hakuwa na asili ya nchi hiyo, Wazazi wake ni raia wa Ireland. So Che alikuwa Muairish.

2 Wakati huo mtu akiitwa 'Che Guevara' ilikuwa ikimaanisha kuwa mtu huyo anaweza kuwa mtu mzuri au mbaya, baadhi ya watu walikuwa wakimwita jina hilo wakimaanisha mpiganaji lakini wengine walimwita hivyo wakimaanisha muuaji.

3. Jina lake la utani lilikuwa Chacho ambalo kwa hapa bongo angeitwa nguruwe, Suala la kuoga kwa Che Guevara lilikuwa mtihani mkubwa. shati na suruali zake alivaa kwa wiki nzima.

4. Hakuwa akipigana kwa njaa na kukosa elimu, aligraduate masomo ya udaktari mwaka 1953. Alitokea katika familia ya kitajiri tofauti na wapiganaji wengi tunaowasoma leo katika historia.

5. Baada ya harakati alikuwa akiweka silaha chini na kutumia mikono hiyo kulea watoto wake, Che alikuwa baba wa watoto watano, mtoto wa kwanza alimzaa na mke wake wa kwanza Hilda Gadea na wengine aliwazaa na mwanamke mwanamapinduzi, Aleida March.

6. Bolivia wanamtukuza wakiamini kuwa Che ni nabii, huko Cuba sura yake ipo kwenye dola tatu na mashuleni kila siku asubuhi watoto hula kiapo wakisema "tunataka kuwa kama Che".

7.kubwa kuliko yote ni kwamba Che alikuwa akipendwa na watu wengi nchini cuba lakini idadi hiyo ililingana na ya watu wanaomchukia.

Mchagga kapata kazi BSS


Jamani, huyu si Master Jay? Haya kulikoni...

Friday, May 29, 2009

Dah, noma kweli...


Jamaa walimkuta dukani kwa Mangi kajificha kwenye boksi ili mangi akifungaaaaa, achukueeeee, wakamaliza humo humo!

ShowLuv...


Kutoka Bagamoyo kwa mshindi wa BSS mwaka jana, Bi Misoji Nkwabi(shoto)kumekuja salamu bendi inafanya mazoezi na hivi karibuni kutakuwa na gig la maana kwa wapenda Sweet reggae, hapa ni shavu na mwanetu Caesar ambaye ni mtangazaji wa shindano hilo mwaka huu, ...asenti!

Thursday, May 28, 2009

UHUSIANO WA UJANANI


Ukipata ujauzito?
...nini kinafuata?

Kaka na dada zangu natumaini hamjambo na mnaendelea vema na shughuli za ujenzi wa Taifa, wasomaji mahiri kabisa wa ukurasa huu, ahsanteni kwa muda wenu, mimi mzima na maisha ni mafupi kusema ukweli, lakini nitakuwa nakosea nikiacha kuyapa sifa yake, ...matamu!
Shukrani kwa wasomaji wangu wa Zanzibar walioamua kushuka kwenye boti, na kuja moja kwa moja mpaka Tabata Relini kuja kumuona, huyu mwandishi wa makala wanazozipenda, zinazowagusa anafananaje? Walipoondoka kuna neno waliniambia likanifanya niwe mpole kidogo, unajua walisemaje? Hata siku moja, usithubutu kumkadiria mtu kwa kumtazama. Utakuwa umekosea sana!
Haya, tuachane na hizi kazi za Mungu, naomba leo tuangalie mambo makubwa yanayothusu sisi vijana wa kike na kiume wa kiAfrika, nazungumzia suala la ujauzito leo. Mmeamua kuwa mtu na mpenziwe, ikafikia hatua sijui ndio tuseme mlijisahau, au nini, ni kitu gani cha kwanza mtafikiria kufanya? Au huwa mnajihisii nini mkifikia hatua hili likatokea kaka na dada zangu?
Kusema ukweli jamani, mengi hufikiriwa hapa, kuna watu hufikia hatua ya kutoroka hata makwao, wakihofia ukali wa wazazi wao, au wakihofia aibu kwa umma, imani ni kwamba, mimba nje ya ndoa ni dhambi ya uzinzi, ambayo kiukweli jamii ikijua kwamba unaifanya bila haya haya, linaweza kuwa tatizo.
Mimi nina yangu ambayo nayafikiria katika hili, naomba nipewe wasaa nianze kumwaga vipengele vyangu. Si sawa jamani:

1. Sio ajabu, ..kawaida...
Ukweli uko hivi, kile kitendo tu cha kuwa wapenzi, kwa utamaduni yetu wa kiafrika, iko bayana kwamba uhusiano huu unahusisha pia tendo la ndoa, ambalo mwishilio wake ndio huu, hasa mkiwa sio watu wa kutumia kinga ya aina yeyote. Tunaelewana, kwa hiyo kwa kushiriki tendo la ndoa, suala la kupata ujauzito lina uwezekano mkubwa hapo jamani, nadanganya?
Sasa cha ajabu nini hapo? Umepanda mpunga, mchele ndio huo. Aibu inatoka wapi wakati ulikuwa pengine unafurahia, kinachofuata hapo ni jinsi ya kukabiliana na tatizo lenyewe, kama kweli wewe unaliona tatizo. Lakini kusema kwamba sijui hukutegemea, unajidanganya mwenyewe, kwa kuwa asilimia kubwa, ni watu wanaojua wanachokifanya. Na kama ulikuwa huutaki huu ujauzito, mbona hata tahadhari hukuchukua? Uliutaka bwana!
Atakayekucheka pia atakuwa mjinga, maana waliozaliwa nje ya ndoa siku hizi ni wengi kuliko hata waliozaliwa ndani ya ndoa, unatakiwa kujipanga hapa na jinsi ya kukabiliana na tatizo lenyyewe, ni lako na hutakuwa na pa kulikimbiza, ...unalo hilo!

2. Haichochei chochote!
Kuna akinadada bwaba huamini kwamba ukim'bebea mtu mimba basi kuna uwezekano mkubwa akawa ndio wako wa maisha. Naomba kuchukua wasaa huu kuwatahadharisha dada zangu kwamba hili si kweli kwamba kunibebea ujauzito, kunaweza kunihamasisha mimi kukuoa, au labda kuishi na wewe kama mtu na mwenzake,...kwa akili zetu vijana wa siku hizi, unaweza kuwa unanikimbiza. Tunaogopa majukumu kuliko tunavyoyaogopa magonjwa ya zinaa, ...mdio ukweli mdio ,maana sioni aibu kulisema hili kwa watu. Si tunajijua?
Nimelisema makusudi maana wanaolalamika mtaani wako wengi, ya kwamba wamekimbiwa, huamua tu kubeba mimba bila ya kuwaambia wenzao, kisha huwashtukiza. Jamaa sasa mara nyingi sijui ndio kusema hawajajiandaa na maisha ya malezi, hukataa, au kukimbia kabisa mji. Ukiangalia sio busara lakini sasa utafanyaje na ndio ushakimbiwa?
Tunabakia pale pale pa kukubali matokeo na kuangalia nini cha kufanya baada ya yote hayo.

3. Unaua? ...ni dhambi zaidi!
Hili ni kimbilio la wengi, kukimbilia kutoa akiamini kwamba amemaliza tatizo, kumbe ndio anajitengenezea matatizo zaidi maana duniani kama mlikuwa hamjui, ni Mungu ametuleta, amekupa uwezo wa kupata kiumbe, unakiua, unafikiri unamfurahisha? We ngoja matokeo yake, hukumu siku hizi iko hapa hapa duniani kama mikuwa hamjui.
Hii ni ya kiimani zaidi, fikiria umefanya dhambi ya uzinzi, hutosheki nayo unaenda kuua tena, halafu huyu Mungu unamuangaliaje? Baso utamtaka msaada? Bado utasema maisha yako yamekosa baraka na utakuwa unahisi kama unaonewa hivi, jibu mwenyewe kabla hatujafunga kurasa.
Kutoa mimba ni hatari kwa afya, na kwa kweli hata kiimani ni mbaya kwa hiyo ushauri wangu ni kwamba, kama unahisi kwamba huko tayari jamani kinga mbona zimejaa kibao? Shauriana na mwenzako au kama vipi acha kabisa haya mambo kama huko tayari nayo.
Mimi hapa kwa leo ndipo nahisi niishie, nataka kuwasiliana zaidi na watu wangu mniambie kuhusiana na hili mnaonaje? Niandikieni email:
Mdimu@hotmail.com
Simu:
+255 787 000 880

Kesho baba kesho....


Ndani ya Irish Pub kama kawaida Banana na Dingi yake Mzee Zahir Zorro, pamoja na B Band nzima, watakuwa wanapiga njaa mpaka jua litoke, kiingilio ni buku tatu tu.
....toleka!

Sinza, ...kumekucha!


Haya tena, watu na njaa zao, ule msimu wa Mamiss umefika na tayari mazoezi yameanza pale Vatican, waratibu ni wale wale, karibuni mjionee vimwana, maana shindano liko mbali, mpaka tarehe 18 bwana...

Njaa mbaya...


Uliza hapa tunapiga nini na wapi? Mbeya Mzee, tumegundua kumbe Kitimoto ina Supu?


Kila mtu alishughulika kudadadeki....