Tuesday, September 25, 2007
...Mudhihir...
...hatimaye Mudhihir anaonekana kama aliyemaliza tiba, hapa akitoka katika Hospitali ya Muhimbili ambako alilazwa kwa matibabu kwa siku kadhaa, tumuombee apone haraka, na kuendelea kulitumikia jimbo lake la Mchinga...
..keshawasili...
Mheshimiwa Juma Kapuya ambaye jana aliripotiwa kupata ajali huko Tabora ambapo watu watatu waliokuwamo kwenye gari lake walipoteza maisha, akishushwa kutoka kwenye Ndege baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam kwa matibabu zaidi, ambapo kwa sasa amelazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili
Sea Cliff...
Kapuya hoi!
Monday, September 24, 2007
Dongo jingine kwa TID
Saturday, September 22, 2007
Mastaa wetu...
MTV Veejay wa Bongo!
Shindano la MTV Veejay limefika ukingoni wanangu na huyu mdada kushoto anayeitwa Vanessa kutoka Arusha ndio kala shavu hilo, na ataaza kuonekana kwenye macho ya watu huko mbele kuanzia mwishoni mwa mwezi huu, tulikula raha kweli Club Maisha jana, ...nakuletea picha zaidi watu wazima tulivyojiachia Ki VIP...
Boyfriend & Girlfriend
Hivi, unajituma au unataka kutumikiwa?
Jamani imefika ile jumamosi ambayo kuna watu wengi wananiambia kwamba huwa wanaisubiri sana, eti waangalie nimesema nini leo? Jamani hivi mnajua kwamba sasa hivi nakuwa napata wakati mgumu sana ninapofikiria kufanya jambo? na hii ni kwa sababu kuna watu wengi makini wananisoma kwa sasa.
Shukrani za dhati kwa wasomaji wangu wa Arusha, ..tulikutana bwana tukajadili mengi tu na tulifurahi kwa kweli kuonana, wengi walishani watakutana na jibaaaaba hilo, kumbe kakijana tu lakini wengi wameniombea, kila mtu kwa imani yake kwamba Mungu anijaalie busara zaidi, maana ninayosema huwa hayalingani na umbo langu na miaka niliyonayo, eti wanadai naongea maneno ya kijana mwenye umri wa miaka 40, ...jamani!
Tuendelee na ya leo maana hizi sifa nikianza kuzielezea wala haziishi, ...kaka na dada zangu, nimesukumwa kuandika haya ninayoandika leo, kuna watu wananiandikia malalamiko kila kukicha. lawama kwa wapenzi wao wakidai kwamba hawaoni kama wanapendwa, yaani wenzi wao hao hawajitumi kabisa katika mapenzi, lakini kuna jibu nikawaandikia, ambalo liliwafanya wanyamaze, unajua niliwauliza nini?
Sawa hao wenzenu hawajitumi, na nyie wenyewe, mmeonesha jitihada gani kuwaweka karibu, ama mnataka kutumikiwa? Kwani jamani mapenzi ni kupenda ama kupendana? Maana wewe unasema huoni dalili kutoka kwa mwenzako, wewe zako ulionesha zikawekwa benchi? sasa kuna utaratibu wa kuangalia katika haya mapenzi, hasa kwa wale ambao walifuatwa, na sio wao kufuata, mnatakaiwa kujua mambo flani ambayo nitawawekea katika vipengele. Tupo p amoja jamani? ..me naanza:
1.Mapenzi na kuamua!
Hili ni jambo ambalo wengi wa vijana waliokuwemo katika uhusiano mlikuwa hamjalifahanu basi habari ndiyo hiyo. mapenzi ya kutegeana yamepitwa na wakati na ni kujidhulumu na mwisho wa siku utajikuta huridhiki na kila unayemuona maana utagundua kwamba labda hakuopendi kumbe wenyewe mnategeana na mwisho wa siku mnajikuta mnahisiana vibaya baada ya kila mtu kutegea kumuona mwenzake akiwa kajitoa kwa mwenzake.
Kama umeshaamua kwamba wewe uko na fulani haina kutegea kaka ama dada yangu. Umeamua kupenda, penda moja kwa moja, na hatua ya kwanza katika hili ni kufukia mashimo. Uliza kivipi? Unapoona anakosea rekebisha, unapohisi hupendi mambo fulani, ambayo mwenzako anayafanya, mwambie ukweli, na kwa kuwa yeye anakupenda anajirekebisha, wazungu wanasema, 'Love makes things happen', na mimi nawaunga mkono, nimeshuhudia watu wakiacha pombe, wakiacha sigara, wakiacha hata umbea kwa sababu ya mapenzi.
Lakini ukitega, kila mtu utamuona ana tabia mbaya, na kumbe tabia mbaya unayo wewe. na kibaya zaidi sasa, unajikuta umeachana na huyu, umeanza na huyu, ukaenda kwa huyu na huyu na yule na mwisho wa siku umefanya msuruuuru wa watu katika uhusiano wako wa kimapenzi. Na dunia si unaijua ilivyofunyangwa na teknolojia. Ndio yaleeee, unaingia mahala unakuta katika watu kumi, wanne umeshakaa nao mkao wa kimapenzi? Heshima ipo hao?
Unajinyima mwenyewe uhuru wa nafsi unakuwa, au nadanganya? ...semeni...
2. mapenzi huambatana na amani ya moyo?
Ndio maana hapo mwanzoni nikawaambia kwamba ukiamua kufanya uhusiano amua tu moja kwa moja maana uhusiano wa kuchungulia chungulia unakuwa kama hujiamini hivi, unakuwa na moyo wa kusita sita, kuliko kufanya hivi ni bora kuacha kaka au dada yangu maana hutafurahia, utakuwa kama unajinyima haki yako ya msingi.
Sasa mambo ya kukaa kama bosi na kusubiri mwenzako ahangaike ndio nini. Na yeye kwa kukuona hivyo unataka kusujudiwa unadhani atakubali kufanywa mjinga, na yeye huenda akawa na mtu anamnyenyekea, atahisi kwamba kwako hamna mapenzi. Kumbe yawezekana yamo, ila sasa tatizo ni kwamba, unasikilizia kwamba kama kweli lipo, ...ndio unakuta muda unakwenda, mmoja ataona anayeyushwa, mara uhusiano unabomoka, ...kila mtu kivyake!
Unatakiwa kabla ya kumwambia mtu I love you too, umehakikisha kabisa kutoka moyoni mwako kama umeamua na moyo ukiamua kupenda unakuwa na amani na ule uhusiano ambao unauanza. Unaona bwana na ukipata baraka kutoka moyoni mwako, penzi la namna hii hudumu asikudanganye mtu na ukihisi moyo unasita, achana na huo uhusiano, utakupotezea muda bila mwenyewe kujijua, na kama huniamini jaribu, ..haufiki popote uhusiano wa namna hii.
3.Nyie tu na mambo yenu
Kuna kosa kubwa ambalo vijana hulifanya pindi wanapokuwa katika husiano zao. Hupenda sana mambo mawili, moja ni kupenda sana kushirikisha rafiki zao katika husiano zao, yaani kuanzia kwenye maamuzi ama katika jambo ambalo wenyewe huliita ushauri kumbe wanakuwa wanauza silaha za maisha yao. Kikulacho ki nguoni mwako kama ulikuwa hujui, ..we una uhakika gani huyo unayemuomba ushauri anafurahia maisha yako na mpenzio?
Hili ni moja jingina bwana, ni lile la kulinganisha mambo, kwamba mbona flani anafanyiwa hiki mi sifanyiwi? Maisha ni kama vidole mikononi mwako, hayawezi kulingana, kuna aina ya maisha ambayo Mungu amekupangia, unatakiwa kukubali hali uliyonayo na kuirekebisha kwa zana ambazo ziko ndani ya uwezo wako, unaona bwana? ukilazimisha tu unakuwa umeharibu kila kitu.
Nomba niwashauri kitu kaka na dada zangu, rafiki yako mkubwa awe mpenzi wako, kama kweli unampenda, yeye ndio mshirikishe kwenye mambo yako na mwisho wa siku utakuja kuona, kila kitu kitanyooka, unajua hii itatoka wapi? ...katika kuhakikisha kwamba mnaridhiana.
Umri unaenda mbele ndugu zangu, hili nawaambia kila siku, mnafikiri bado tuna muda wa kupoteza vijana wenzangu? Mangapi yanatusubiri kwa ajili ya maisha yetu ya baadae?
Naomba niishie hapa kwa leo ndugu zangu, nina imani somo mmelipata na kama mna la zaidi la kuniambia, naomba mniandikie kule kwenye:
HMdimu@Mwananchi.co.tz
+255 787 000 880
Wiki ijayo, ...nipo hapa hapa, ..msikose.
Jamani imefika ile jumamosi ambayo kuna watu wengi wananiambia kwamba huwa wanaisubiri sana, eti waangalie nimesema nini leo? Jamani hivi mnajua kwamba sasa hivi nakuwa napata wakati mgumu sana ninapofikiria kufanya jambo? na hii ni kwa sababu kuna watu wengi makini wananisoma kwa sasa.
Shukrani za dhati kwa wasomaji wangu wa Arusha, ..tulikutana bwana tukajadili mengi tu na tulifurahi kwa kweli kuonana, wengi walishani watakutana na jibaaaaba hilo, kumbe kakijana tu lakini wengi wameniombea, kila mtu kwa imani yake kwamba Mungu anijaalie busara zaidi, maana ninayosema huwa hayalingani na umbo langu na miaka niliyonayo, eti wanadai naongea maneno ya kijana mwenye umri wa miaka 40, ...jamani!
Tuendelee na ya leo maana hizi sifa nikianza kuzielezea wala haziishi, ...kaka na dada zangu, nimesukumwa kuandika haya ninayoandika leo, kuna watu wananiandikia malalamiko kila kukicha. lawama kwa wapenzi wao wakidai kwamba hawaoni kama wanapendwa, yaani wenzi wao hao hawajitumi kabisa katika mapenzi, lakini kuna jibu nikawaandikia, ambalo liliwafanya wanyamaze, unajua niliwauliza nini?
Sawa hao wenzenu hawajitumi, na nyie wenyewe, mmeonesha jitihada gani kuwaweka karibu, ama mnataka kutumikiwa? Kwani jamani mapenzi ni kupenda ama kupendana? Maana wewe unasema huoni dalili kutoka kwa mwenzako, wewe zako ulionesha zikawekwa benchi? sasa kuna utaratibu wa kuangalia katika haya mapenzi, hasa kwa wale ambao walifuatwa, na sio wao kufuata, mnatakaiwa kujua mambo flani ambayo nitawawekea katika vipengele. Tupo p amoja jamani? ..me naanza:
1.Mapenzi na kuamua!
Hili ni jambo ambalo wengi wa vijana waliokuwemo katika uhusiano mlikuwa hamjalifahanu basi habari ndiyo hiyo. mapenzi ya kutegeana yamepitwa na wakati na ni kujidhulumu na mwisho wa siku utajikuta huridhiki na kila unayemuona maana utagundua kwamba labda hakuopendi kumbe wenyewe mnategeana na mwisho wa siku mnajikuta mnahisiana vibaya baada ya kila mtu kutegea kumuona mwenzake akiwa kajitoa kwa mwenzake.
Kama umeshaamua kwamba wewe uko na fulani haina kutegea kaka ama dada yangu. Umeamua kupenda, penda moja kwa moja, na hatua ya kwanza katika hili ni kufukia mashimo. Uliza kivipi? Unapoona anakosea rekebisha, unapohisi hupendi mambo fulani, ambayo mwenzako anayafanya, mwambie ukweli, na kwa kuwa yeye anakupenda anajirekebisha, wazungu wanasema, 'Love makes things happen', na mimi nawaunga mkono, nimeshuhudia watu wakiacha pombe, wakiacha sigara, wakiacha hata umbea kwa sababu ya mapenzi.
Lakini ukitega, kila mtu utamuona ana tabia mbaya, na kumbe tabia mbaya unayo wewe. na kibaya zaidi sasa, unajikuta umeachana na huyu, umeanza na huyu, ukaenda kwa huyu na huyu na yule na mwisho wa siku umefanya msuruuuru wa watu katika uhusiano wako wa kimapenzi. Na dunia si unaijua ilivyofunyangwa na teknolojia. Ndio yaleeee, unaingia mahala unakuta katika watu kumi, wanne umeshakaa nao mkao wa kimapenzi? Heshima ipo hao?
Unajinyima mwenyewe uhuru wa nafsi unakuwa, au nadanganya? ...semeni...
2. mapenzi huambatana na amani ya moyo?
Ndio maana hapo mwanzoni nikawaambia kwamba ukiamua kufanya uhusiano amua tu moja kwa moja maana uhusiano wa kuchungulia chungulia unakuwa kama hujiamini hivi, unakuwa na moyo wa kusita sita, kuliko kufanya hivi ni bora kuacha kaka au dada yangu maana hutafurahia, utakuwa kama unajinyima haki yako ya msingi.
Sasa mambo ya kukaa kama bosi na kusubiri mwenzako ahangaike ndio nini. Na yeye kwa kukuona hivyo unataka kusujudiwa unadhani atakubali kufanywa mjinga, na yeye huenda akawa na mtu anamnyenyekea, atahisi kwamba kwako hamna mapenzi. Kumbe yawezekana yamo, ila sasa tatizo ni kwamba, unasikilizia kwamba kama kweli lipo, ...ndio unakuta muda unakwenda, mmoja ataona anayeyushwa, mara uhusiano unabomoka, ...kila mtu kivyake!
Unatakiwa kabla ya kumwambia mtu I love you too, umehakikisha kabisa kutoka moyoni mwako kama umeamua na moyo ukiamua kupenda unakuwa na amani na ule uhusiano ambao unauanza. Unaona bwana na ukipata baraka kutoka moyoni mwako, penzi la namna hii hudumu asikudanganye mtu na ukihisi moyo unasita, achana na huo uhusiano, utakupotezea muda bila mwenyewe kujijua, na kama huniamini jaribu, ..haufiki popote uhusiano wa namna hii.
3.Nyie tu na mambo yenu
Kuna kosa kubwa ambalo vijana hulifanya pindi wanapokuwa katika husiano zao. Hupenda sana mambo mawili, moja ni kupenda sana kushirikisha rafiki zao katika husiano zao, yaani kuanzia kwenye maamuzi ama katika jambo ambalo wenyewe huliita ushauri kumbe wanakuwa wanauza silaha za maisha yao. Kikulacho ki nguoni mwako kama ulikuwa hujui, ..we una uhakika gani huyo unayemuomba ushauri anafurahia maisha yako na mpenzio?
Hili ni moja jingina bwana, ni lile la kulinganisha mambo, kwamba mbona flani anafanyiwa hiki mi sifanyiwi? Maisha ni kama vidole mikononi mwako, hayawezi kulingana, kuna aina ya maisha ambayo Mungu amekupangia, unatakiwa kukubali hali uliyonayo na kuirekebisha kwa zana ambazo ziko ndani ya uwezo wako, unaona bwana? ukilazimisha tu unakuwa umeharibu kila kitu.
Nomba niwashauri kitu kaka na dada zangu, rafiki yako mkubwa awe mpenzi wako, kama kweli unampenda, yeye ndio mshirikishe kwenye mambo yako na mwisho wa siku utakuja kuona, kila kitu kitanyooka, unajua hii itatoka wapi? ...katika kuhakikisha kwamba mnaridhiana.
Umri unaenda mbele ndugu zangu, hili nawaambia kila siku, mnafikiri bado tuna muda wa kupoteza vijana wenzangu? Mangapi yanatusubiri kwa ajili ya maisha yetu ya baadae?
Naomba niishie hapa kwa leo ndugu zangu, nina imani somo mmelipata na kama mna la zaidi la kuniambia, naomba mniandikie kule kwenye:
HMdimu@Mwananchi.co.tz
+255 787 000 880
Wiki ijayo, ...nipo hapa hapa, ..msikose.
Hili hapa...
Full kujiachia...
Weekend hii bwana., watu wanajiachia, hawa ni wadau wa muziki wa kizazi kipya bwana, watoto wa TNG, wakiwa na Joh Makini, kushoto kabisa. B12 wa nne kutoka kushoto, na kisha Lord Eyes wa nako2Nako na mwisho kabisa mtoto anaitwa Makamua, ana traki lake linaitwa Why kwa sasa amempa shavu mtu mzima ChidBeeeeenz!
Thursday, September 20, 2007
Watoto wa Msimbazi!
Taifa Mademu
Wednesday, September 19, 2007
Hapo VP?
Life Oooh life...
Waitara kaaga!
Tuesday, September 18, 2007
Majibu kutoka kwa Dingi!
Naota...
Jobu kwa Ben
Mafundi..
Majaji...
Saturday, September 15, 2007
Boyfriend & Girlfriend
Penzi la kuibia tamu? Nani kakwambia?
Jamani, duniani kuna mambo, haya, na tuanze kwa kumshukuru Mungu kwa kuweza kuturuhusu tukutane tena Jumamosi hii na kuchukua muda wetu mchache kuongea angalau kwa uchache kuhusiana na suala zima la mahaba, mimi mzima, hofu na mashaka ni juu yenu nyie mlio mbali na upeo wa macho yangu. Ila nina imani mmesalimika!
Leo nina mada ambayo nilikuwa nimekaa kijiweni Ijumaa iliyopita, nikawakuta watu wazima na akili zao wanaijadili huku wakiipa sifa kweli hali ya penzi la kuibia, kwamba lina utamu uliopitiliza, nilipobisha, nikaambiwa usisikie, usiombe ukajaribu, unaweza ukagombea kuwa mwenyekiti wa chama cha wezi wa wake za watu!..nikaondokamahala pale maana nikahisi ningesikiliza sana ningeshawishika, ..mjue ni dhambi halafu madhara yako bayana,
Unaona bwana, sasa katika tafakuri yangu kuna mambonimeyagundua, kwa asiye naakili timamu anaweza akasema kwamba kuna faida nyingi atapata ambazo nitazisema kwa mafungu kama kawaida yangu na nitaongelea asthari katika kipengele cha mwisho kabisa.
1. Halina gharama!
Unaona bwana, watu wengi ambao ni wezi wa wake za watu hulifurahia penzi la wizi kwa kuwa hutunziwa hawa wanawake, yaani mwenye mke anapendezesha, amalisha na kila kitu, yeye kazi yake inakuwani kufurahia penzi tu ambalo halionei uchungu kwa hiyo yeye anakuwa anafaidi zaidi kuliko mwenye mali.
Kama anaingia gharama utakuta ni ya simu ya kumpigia, au kama wanakutana mahala mamb ya chakula na malazi kama wataamua kulala jambo ambalo ni sawa na hakuna kuliko ambavyo kama angekuwa na mtu ambaye labda angekuwa anamhudumia.
Hii ni mojawapo ya raha ambayo wezi wa wake za watu wanaifurahia na ni sababu ya msingi kiasi fulani inayopelekeawao kusema ni kwa nini penzi la kuiba ni tamu...
2. Penzi moto!
Kuna ujinga ambao naamini kabisa kuna wanandoampaka leo wanaufanya, nao ni kujifanya wana heshima saaaana baina yao, hata katika masuala ya mapenzi. Kifupi hawako wazi, wanakuwa wanakificha kile ambacho wanakipenda sana wanapokuwa mahabani, matokeo yake utakuta mtu tangu anaingia kwenye ndoa, mpaka anapata watoto, anakuwa hafurahii kabisa mahaba na mumewe.
Sasa ndio usiombe akaja akakutana na huyu mwizi ambaye atataka kuonesha maujuzi yake ili amteke mwenzako kiakili, ....utajuta!
Mara nyingi mapenzi ya namna hii ya kuiba watu huwa huru kufanyiana kila upuuzi unaohusianan a mapenzi, na hapa ndio utamu unapoanzia. Kingine penzi moto litakuja pale ambapo mtu anaudhiwa huko nyumbani, wanakuwa wanalala 'Mzungu wa nne', huyu ndio huko anakoiba ama kuibiwa anamalizia usongo wote!
....pata picha mwenyewe!
3. Haina kero..yaani shwari tu!
Unajua kuna jambo moja baina yetu wanadamu, mpaka watu mgombane, lazima mtakuwa kwa kiasi fulani mezoeana, sasa hawa wanaoibana mara nyingi huwa wanapatana sana maana muda wa kukaa na kuanza kusomana huwa hawana, hawa mara nyingi wakikutana wanakuwa na kazi moja tu, mahaba moto moto kisha wakimaliza kila mtu anaishia kivyake.
Tofauti na wenye husiano za kudumu, kunakuwa na migogoro iliyoongozana. Kila mara wanakuwa wanagombana na hii mara nyingi inakuwa ni kero baina yao. Na hii ni sababu mojawapo wezi wa mapenzi wanakuwa wanaamini kwamba ni bora penzi la kuibia, kuliko kuwa na uhusiano na mtu.
Maana kingine ni kwamba si unajijua ni mwizi? Kwa hiyo hata kuchunga sana unakuwa huna haja, mwenye mke si atakuwa analindakwa niaba? Sasa wewe presha za nini?
Mimi kwa leo naona niishie hapa, wiki ijayo ndio nitakupa madhara ya kuibia penzi, lakini kama una maoni tuma ujumbe kwenye namba +255 787 000 880 uniambie au kwa email:
Mdimu@hotmail.com
Jamani, duniani kuna mambo, haya, na tuanze kwa kumshukuru Mungu kwa kuweza kuturuhusu tukutane tena Jumamosi hii na kuchukua muda wetu mchache kuongea angalau kwa uchache kuhusiana na suala zima la mahaba, mimi mzima, hofu na mashaka ni juu yenu nyie mlio mbali na upeo wa macho yangu. Ila nina imani mmesalimika!
Leo nina mada ambayo nilikuwa nimekaa kijiweni Ijumaa iliyopita, nikawakuta watu wazima na akili zao wanaijadili huku wakiipa sifa kweli hali ya penzi la kuibia, kwamba lina utamu uliopitiliza, nilipobisha, nikaambiwa usisikie, usiombe ukajaribu, unaweza ukagombea kuwa mwenyekiti wa chama cha wezi wa wake za watu!..nikaondokamahala pale maana nikahisi ningesikiliza sana ningeshawishika, ..mjue ni dhambi halafu madhara yako bayana,
Unaona bwana, sasa katika tafakuri yangu kuna mambonimeyagundua, kwa asiye naakili timamu anaweza akasema kwamba kuna faida nyingi atapata ambazo nitazisema kwa mafungu kama kawaida yangu na nitaongelea asthari katika kipengele cha mwisho kabisa.
1. Halina gharama!
Unaona bwana, watu wengi ambao ni wezi wa wake za watu hulifurahia penzi la wizi kwa kuwa hutunziwa hawa wanawake, yaani mwenye mke anapendezesha, amalisha na kila kitu, yeye kazi yake inakuwani kufurahia penzi tu ambalo halionei uchungu kwa hiyo yeye anakuwa anafaidi zaidi kuliko mwenye mali.
Kama anaingia gharama utakuta ni ya simu ya kumpigia, au kama wanakutana mahala mamb ya chakula na malazi kama wataamua kulala jambo ambalo ni sawa na hakuna kuliko ambavyo kama angekuwa na mtu ambaye labda angekuwa anamhudumia.
Hii ni mojawapo ya raha ambayo wezi wa wake za watu wanaifurahia na ni sababu ya msingi kiasi fulani inayopelekeawao kusema ni kwa nini penzi la kuiba ni tamu...
2. Penzi moto!
Kuna ujinga ambao naamini kabisa kuna wanandoampaka leo wanaufanya, nao ni kujifanya wana heshima saaaana baina yao, hata katika masuala ya mapenzi. Kifupi hawako wazi, wanakuwa wanakificha kile ambacho wanakipenda sana wanapokuwa mahabani, matokeo yake utakuta mtu tangu anaingia kwenye ndoa, mpaka anapata watoto, anakuwa hafurahii kabisa mahaba na mumewe.
Sasa ndio usiombe akaja akakutana na huyu mwizi ambaye atataka kuonesha maujuzi yake ili amteke mwenzako kiakili, ....utajuta!
Mara nyingi mapenzi ya namna hii ya kuiba watu huwa huru kufanyiana kila upuuzi unaohusianan a mapenzi, na hapa ndio utamu unapoanzia. Kingine penzi moto litakuja pale ambapo mtu anaudhiwa huko nyumbani, wanakuwa wanalala 'Mzungu wa nne', huyu ndio huko anakoiba ama kuibiwa anamalizia usongo wote!
....pata picha mwenyewe!
3. Haina kero..yaani shwari tu!
Unajua kuna jambo moja baina yetu wanadamu, mpaka watu mgombane, lazima mtakuwa kwa kiasi fulani mezoeana, sasa hawa wanaoibana mara nyingi huwa wanapatana sana maana muda wa kukaa na kuanza kusomana huwa hawana, hawa mara nyingi wakikutana wanakuwa na kazi moja tu, mahaba moto moto kisha wakimaliza kila mtu anaishia kivyake.
Tofauti na wenye husiano za kudumu, kunakuwa na migogoro iliyoongozana. Kila mara wanakuwa wanagombana na hii mara nyingi inakuwa ni kero baina yao. Na hii ni sababu mojawapo wezi wa mapenzi wanakuwa wanaamini kwamba ni bora penzi la kuibia, kuliko kuwa na uhusiano na mtu.
Maana kingine ni kwamba si unajijua ni mwizi? Kwa hiyo hata kuchunga sana unakuwa huna haja, mwenye mke si atakuwa analindakwa niaba? Sasa wewe presha za nini?
Mimi kwa leo naona niishie hapa, wiki ijayo ndio nitakupa madhara ya kuibia penzi, lakini kama una maoni tuma ujumbe kwenye namba +255 787 000 880 uniambie au kwa email:
Mdimu@hotmail.com
ShowLove!
Kala amekula!
Unamkumbuka huyu jamaa? Anaitwa Kala Jeremiah, alikuwammoja kati ya washirikiwa Bongo Star Search mwaka jana,akashika nafasi kama ya nne hv, ..mwaka huu amek\kula shavu lautangazaji kwenye hiiTour ya kusaka vipaji ambayo wiki iliyopita ilikuwa Zanzibar, na leo mambo yanaendelea pale Blue Tripple A, ...kuna nyomi...
Safari imeanza!
Monday, September 3, 2007
..tutafanyaje sasa?
jamani!
Sunday, September 2, 2007
Jamani Doooooktaaaa!
Anashika hapa kudadadeki...heeeehe!
Saturday, September 1, 2007
Kama Wembley kudadadeki!
Mapemaaaaaaa
Balozi wa Redds
Shavu
Na huyu ndio....
Mzee Kawawa ndani!
Majaji
Miss Tanzania
Subscribe to:
Posts (Atom)