Friday, January 8, 2010

Man X, ..huyu hapa!


Msanii mkongwe katika mziki wa kizazi kipya Alex Kushaba a.k.a Man X ameamua kujitosa rasmi katika kundi la TMK Majita original baada ya kufanya nao kazi kwa muda mrefu.
“Nimeona na vyema kujikita moja kwa moja na kundini kwani naamini kwa pamoja tutafika mbali”
Mpaka hivi sasa ameshafanya nyimbo mbili na kundi hilo na kuwa amejipanga vizuri zaidi kwa ajili ya kazi moja tu ya kutoa burudani kwa wapenzi wa muziki.
Kiongozi wa kundi hilo Eno K alisema kuwa wameamua kushirikiana na Man X kwa kuwa yeye ni mkali na ni mshikaji wao toka kitambo.
Kundi la TMK Majita Original llianzishwa miaka saba iliyopita maeneo ya keko mpaka sasa linamebaki na wasanii tofauti tofauti akiwemo Eno K, Fid, Soulder, Kindago, Jose, Kamoja, Dibwizzle pamija na Man x.

No comments: