Saturday, January 2, 2010

KGT: 2010, ..ni kazi tu...


Kama haujawahi kukutana na KGT halafu ukakutana naye kwa mara ya kwanza, sidhani kama unaweza kuamini kuwa yeye ndo aliye’produce album bora ya mwaka katika tuzo za kill music awards, Cinderela ya Ali Kiba, ni kijana mwenye umbo dogo asiye na makuu.
Jina lake ni Omari Said Kombo maarufu kama KGT…. Usijiulize sana kirefu chake kwani yeye mwenyewe anasema KGT haina maana yoyote.
Ni audio producer kama walivyo kina Marco Chali, P Funk ns wengine, lakini pia wakati mwingine huikamata maiki, anamiliki nyimbo kadhaa nyumbani kwake.
Cha kushangaza nyimbo anazofanya yeye na kuimba yeye mwenyewe ‘hazipati air time’ ya kutosha lakini anazowafanyia watu ndugu yangu zinapata air time si kitoto kwakweli, baadhi ya nyimbo alizoimba ni ‘ One day’ na ‘something about you’.
Baadhi ya wasanii alipfanya nao kazi na anaoendelea kufanya nao kazi ni Ali Kiba, Pasha, Queen Darleen, Showdady, Manyota, Taqwa na Berry white ambao wengi wao amewafanyia albamu mzima.
Akizungumzia kazi anasema kuwa ni nzuri na inahitaji ‘concentration’ sana….. kuna baadhi ya wasanii ni wabishi hawataki kukubaliana na ukweli…. “ Ila nimejipanga vizuri kupambana kwenye hii ‘industry’ na naamini mwaka huu nitatoa albamu bora kama sio nyimbo bora.”

No comments: