Tuesday, January 5, 2010

Kitu kipya, ..kutoka Tetemesha records...


Tetemesha Recordz inauanza mwaka 2010 kwa kumtambulisha artist wake mpya ambaye hajawahi kuskika. Anaitwa SAJNA, ni msanii mwenye miaka 18, anasoma form II hapa Mwanza. Kijana ana kipaji cha hali ya juu.
Ana wimbo, ..wimbo huu unaitwa NADHIFA, ni true story ambayo imemtokea yeye mwenyewe, kila alichokiimba katika wimbo huu ni cha kweli na kinamhusu yeye na familia yake.
Kwa ufupi amemuimba dada yake wa damu ambaye alitoweka nyumbani kwao bila taarifa miaka kadhaa iliyopita.
Wimbo umetengenezwa A2P RECORZ MWANZA, producer anaitwa SAM TIMBER.

No comments: