Saturday, January 2, 2010

Bongo kuna wanamuziki?


MBUNGE wa jimbo la Mbinga na kiongozi wa bendi ya TOT, Kapteni John Komba amesema bongo hakuna wanamuziki bali kuna wasanii.
Anasema mwanamuziki anauwezo wa kuandika nyimbo na ikaimbwa na mwanamuziki yeyote duniani, lakini msanii ni mbabaishaji tu kama waliopo hapa bongo hawajui ‘notation’ nota za muziki.
Komba amesema mwanamuziki ni lazima ajue nota za muziki kama hajui ni msanii na kwa maana hiyo ni mbabaishaji na wanamuziki wengi wa bongo hawazijui.
“Mfano ninaweza kukwambia kuwa hule wimbo wa ‘We are the World’ uliandikwa na mwanamuziki ndiyo maana wanamuziki wengi namna hile waliimba bila kubabaika kwa sababu wanajua nota za muziki” anasema Komba.
Komba anasema anawaomba wasanii wa bongo waweze kuzisoma nota za muziki ili waweze kuwa wanamuziki wa ukweli.

No comments: