Wednesday, May 27, 2009

usilolijua bwn...


1. Umeshawahi kujiuliza hivi nisipooga kwa siku kumi itakuwaje? Ndani kutakalika kweli? Halle Berry amewahi kuishi kwa siku kumi bila kuoga wala kupiga mswaki. Hii ilitokea alipokuwa akiigiza filamu ya Jungle Fever, ama kweli hakuna kazi rahisi anasema.

2.Kama kuna mtu duniani angetamani kumsaidia anasema angependa sana kumsaidia mwanamuziki mahiri wa pop, Britney Spears. Anasema anamwonea huruma sana hasa anapoandikwa kwasababu anayajua maumivu yasababishwayo na vyombo vya habari. "unakuwa umeumia tayari lakini vyombo vya habari vinakuongezea maumivu kwa kukuandika vibaya" anasema

3. Aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na JT( Justine Timberlake) baada tu ya kuachana na Erick Benet mwaka 2003. Hata hivyo uhusiano huo ulikuwa wa muda mfupi sana.

4. Ingawa ukimwangalia huwezi kufikiria kama mwanamke huyo anaweza kufanya upasuaji wa viungo lakini mwenyewe anasema Never say Never anafikiri ipo siku anaweza kufanya upasuaji.

5. Hasimu wake mkubwa ni Charlize Theron hata hivyo anasema hajali sana na huelekeza nguvu zake kwenye kazi na si kwenye mambo kama hayo.

No comments: